Deuteronomy 18:15-18

15 a Bwana Mwenyezi Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye. 16 bKwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mwenyezi Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mwenyezi Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”

17Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema. 18 cNitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
Copyright information for SwhKC